Posts

ELIMU PATAPOTEA!

Image
Picha nikiwa chuo Cha ufundi Mombasa. Kwa kweli,safari ni hatua na kila hatua ni dua.Nina maana gani na kauli hii?Leo hii nimeamua kujitokeza waziwazi na kuiweka paruwanja safari ya masomo yangu ya chuo kikuu.Nikikupakulia na na kuyadadavua kinaganaga usiyoyafahamu kiundani.Asilimia kubwa wakisalia kuwa ni hadithi za Abunwasi na kumbukizi zisizoaminika katu.Waama,kitanda usichokilalia hujui kunguni wake. Masomo ya chuo kikuu ni baadhi ya malengo ya kila adinasi aushini.Nimekuwa mshawasho na ari ya kupata elimu ya vyuo vikuu pindi tu baada ya kukamilisha masomo yangu ya shule ya upili.Nikitaka niyaonje mandhari hayo kwa udi na uvumba kutokana na habari za kutia moyo nilizozipata kutoka kwa watangulizi wangu.Kumbe nilikuwa najipalia makaa. pichani nikiwa kwenye vidato chuo kikuu Cha ufundi Mombasa baada ya kipindi. Maji yalianza kumwagika pindi tu baada ya kusajiliwa chuoni na kukosa vifaa muhimu vikiwemp kipakatalishi na rununu hitajika nikitaja tu baadhi.Iweje n...

VIJANA TAMBARANI!

Image
Picha kwa hisani ya google. Samaki mkunje angali mbichi na mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.Hizi ndizo fikra ambazo hukita mizizi akilini mwetu sie wakenya pindi tu jina "kijana" linapotamkwa.Kwa miaka na Mikaka Sasa taifa la Kenya kupitia serikali tawala imekuwa ikijitokeza kinaganaga na kudai kubuni nafasi zaidi za ajira kwa kizazi cha baadaye ambao ni vijana zilizosalia kuwa ndoto za mchana kutekelezwa.Imesalia tu kama kumbukizi kwa dhana kuwa "kazi kwa vijana....pesa kwa wazee" ikijidhihirisha waziwazi kama meno ya ngiri.Suala Hilo limegeuka na kuwa donda sugu linalopaswa kuzingatia kikamilifu. picha angavu kwa hisani ya google. Wasemavyo walumbi,mgala muuwe na haki umpe.Yapasa husika kuingilia kati na kubuni nafasi mbalimbali za ajira kwa kizazi cha baadaye.Hili litawawezesha kupata kipato cha kujimudu kimaisha.Ikilinganishwa kuwa taifa letu lina idadi kubwa ya vijana, itasaidia pakubwa kuboresha na kuimarisha uchumi kwa jumla.Walinena walu...

CHOZI LA DAMU!

Image
Picha angavu kwa hisani ya mamlaka ya kukabiliana na majanga NDMA.                     Nainamisha kichwa tayari kutema madini, Mara hii nikiwa nimejawa na lindi la mawazo na maswali chungu nzima nisipate hata jawabu.Kulikoni? Wasemavyo walumbi, mbiu ya mgambo ikilia lazima pawe na jambo.Si jambo tu.Ni suala ambalo lafaa litiliwe mkazo na hatua madhubuti kuchukuliwa ili kukabili tatizo hili.Jangwa la ukame limekuwa tishio kubwa nchini huku likikithiri si tu magazetini, kwenye vyombo vya habari na hata semasema za mtaani.                    Jangwa la ukame limekuwa donda sugu nchini kwa miaka na mikaka Sasa.Hayawani, Mifugo na kadhalika wakiachwa hohehahe bila mbele wala nyuma na hivyo kuishia kupoteza uhai kama si kudhoofika kiafya tu.Ni mwaka huu ambapo majimbo mbalimbali yameripotiwa kuathirika.Kaunti hizo ni pamoja na; Baringo, Isiolo, Marsabit, Garissa, Wajir, Mandera, Tana...

TABASAMU TAANUSI KWA WAPWANI!

Image
                Wasemavyo walumbi nyumbani ni nyumbani tu hata kama ni pangoni na kitanda usichokilalia hujui kunguni wake.Imesadifika tu kama hekaya za Abunwasi kwetu sie wapwani huku tukisalia tumeduwaa na kubung'aa falauka mzungu wa reli tusiamini kutokana na furaha chekwachekwa iliojaa moyoni.Walilonga waswahili kuwa,lisemwalo lipo na kama halipo laja.Nakusihi uketi kitako ewe msomaji wangu nikudadavulie yaliyomo!                      Ni miezi miwili tu tangie sie wapwani na wakenya kwa ujumla kushiriki kwenye uchaguzi mkuu wa agosti tisa huku kilio chetu wapwani kikiwa ni halwa tamu tulionyang'anywa kinywani na kupelekewa wakazi wa Naivasha kwenye nia ya huduma za halmashauri ya bandari nchini (KPA).Ama kweli chozi la samaki haliendi bure majini.                  Nakumbuka tu kama jana jinamizi  lililotufyonza sie w...

HALUA CHUNGU VYUONI.

          Naitwaa tena kalamu tayari kumwaya wino,mara hii nikiwa nimesonya na kusononeka moyoni.Kwani kulikoni?Kwa muda Sasa taifa letu la Kenya limekuwa likiitathmini elimu kama sekta adhimu nchini Hasa Sana kwa ukuaji  na uboreshaji wa uchumi.Namaanisha Nini kwa usemi huu?Elimu ya ngazi ya juu imepewa kipaumbele nchini si tu vyuoni bali hadi kwenye taasisi anuwai za masomo.           Sie wakenya tumeingiwa na ukasumba na ukiritimba potovu kuwa wana wetu wakifuzu na kuitwa kwenye vyuo vikuu basi pana tumaini la maisha bora ya baadaye pasi na kufahamu ni yepi hutokea pindi tu wanapojiunga na vyuo hivyo kwa tukisahau kuwa ufanisi huhitaji jitihada,bidii na ukakamavu masomoni.           Kwa sasa elimu ya vyuo vikuu imegeuka na kuwa karaha kwetu sie  wasomi.Mbona hivyo?Sie wanafunzi twajisahau na kujiingiza kwenye lindi la mapenzi na kukosa kutafakari kiini  hasa Cha kujiunga na taasisi hizo.Wengi we...

KILIO CHA WANYONGE.

           Lisemwalo lipo na kama halipo laja.Mbona hivyo?Kwanza,naanza kwa kukupongeza ewe Rais William Ruto kwa kuibuka mshindi kwenye uchanguzi mkuu wa agosti Tisa.Na Sasa macho yote yameelekezwa kwako baada ya kuaminiwa na kutwikwa jukumu la kuongoza baada ya kuyaweka paruwanja manifesto na ajenda zako kwa wakenya achia mbali ukakamavu,ukomavu,hekima na msimamo wako dhabiti wa kisiasa.Heko kwa Hilo.           Mheshimiwa rais,ilidhihirika wazi tu kama meno ya ngiri kwenye sakasaka zako katika safari ya kuingia ikulu wakati ukimrai na kumuahidi "Wanjiku" kuwa utashughulikia mahitaji yake huku maneno kama"mama mboga" na "bodaboda" yakikita Kambi kinywani kwenye Nia ya"bottom up economy",ukimuahidi mlalahoikuwa kwa kipindi siku mia moja pindi tu baada ya kula kiapo,utatekelezs masuala kama kupunguza bei ya bidhaa muhimu ikiwemo unga,kuwateua  majaji zaidi kutaja baaadhi tu.           Kiapo umekila,umefa...